Monday, November 4, 2013

PICHA ZA MATUKIO YA TAMASHA LA EID EL FITRI YA MWAKA 1431

Hakika ilikuwa furaha kwa kila mmoja aliyebahatika kuhudhuria sherehe za Tamasha la Eid el fitr mwaka 1431 Hijria, lakini siku hazirudi nyuma bali zinaenda mbele, bali kumbukumbu ya matukio ya picha ndio yanayoturudisha nyuma kufurahia yale mazuri ambayo yaliyopita, Nafsi zetu kujiuliza hizi sherehe zilikuwa za mwaka 1431 wakati huo kamati ya vijana ya Istiqaama ilikuwa changa mno, je sherehe za Tamasha la Eid 1435 inshaallah zitakuwa katika ubora upi?, miaka 4 imepita tokea Tamasha hili lilipofanyika, kwani Kamati ya vijana Istiqaama imezidi kuwa na uzoefu na hivi sasa ina vijana imara katika kusimamia dini ya Allah s.w, kila mmoja wetu akijaaliwa uhai na afya inshaallah ajitahidi kuhudhuria katika sherehe za Tamasha la Eid el Fitri 1435 mwaka na amtaarifu kila mmoja ambaye hajawahi kuhudhuria sherehe hizo za Tamasha la Eid zinazofanyika katika viwanja vya Dar es salaam ZOO kila mwaka.
Wageni walioalikwa Masheikh kutoka Misri ambao pia ni waalimu wa chuo cha Markaz na Sheikh Al haad Musa ambaye ni Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam


















Hakika zawadi zilikuwa za aina yake ambazo zilizidisha furaha ya sherehe za eid kwa wale walioshinda, huenda inshaallah sherehe zijazo za mwaka 1435 kutakuwa na zawadi ya Flat screen na ikiwepo naona shindano litakuwa la kusisimua mno. 

No comments:

Post a Comment