Thursday, November 14, 2013

Makamu wa Rais wa Tanzania ajumuika na waislamu katika hafla ya kuukaribisha mwaka mpya wa kiislamu 1435 Hijriyyah.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam,  kwa ajili ya kuhudhuria hafla ya kuupokea mwaka mpya wa Kiislamu 1435 Hijriyya huku akilakiwa na waumini, kulia kwake ni wana Kamati ya vijana Sulaiman Sharjiy na Muthanna H. Al Shaibaniy.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia katika hafla ya sherehe za kuukaribisha mwaka mpya wa Kiislamu 1435 Hijriyya
 

Makamu wa Rais akisalimiana na Sheikh Ali Suleiman Al Kharousy, katikati anayeshuhudia ni Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhaad Musa Salum

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisalimiana kwa furaha na Mwenyekiti wa Kamati ya vijana Istiqaama Sheikh Saleh Omar Attiwaaniy huku akishuhudiwa na Sheikh Hafidh Attiwaaniy na Sheikh Ali Suleiman Al Kharousy

Sheikh Saleh Omar akijadiliana jambo na Balozi wa Egypt nchini Mheshimiwa Hossam Moharram

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr. Mohammed Gharib Bilal akipeana mkono na Sheikh Saleh Omar Attiwaaniy na katikati anayeshuhudia ni mtunzi mahiri wa vitabu vya dini ya Kiislamu katika zama hizi Sheikh Khalfan Sulaiman Attiwaaniy Allah S.W amjaalie umri mrefu na wenye kheri na baraka

 Sheikh Saleh Omar akiwa na Mheshimiwa Shamim Khan ambae mchango wake ulikuwa mkubwa katika serikali ya nchi yetu ya Tanzania na pia katika harakati mbalimbali za uislamu nchini.

Sheikh Saleh Omar akipena mkono na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania Mheshimiwa Dr. Gharib Bilal

Wageni waalikwa wakiitikia dua iliyosomwa na Sheikh Ahmed Mohammed Al Badry

 Kumbukumbu ya Picha ya Hafla ya Mwaka 1435 Hijriyya, picha iliyopigwa nje ya Ukumbi wa Karimjee
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhaad Musa Salum akimpa zawadi Makamu wa Rais wa Tanzania kwa kutambua mchango wake katika kufanikisha hafla ya kupokea mwaka mpya wa kiislamu 1435 Hijriyyah

Makamu wa Rais wa Tanzania akijadili jambo na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam

Sehemu ya waumini wa dini ya Kiislamu,waliohudhuria hafla ya kuupokea mwaka mpya wa Kiislamu 1435 Hijriyya, wakiitikia dua iliyosomwa na Sheikh Ahmed Mohammed Al Badry, katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam

 
 Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Mussa Salum, akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Makamu wa Rais, Dkt. Bilal, kuhutubia hadhira iliyofika katika hafla hiyo.

No comments:

Post a Comment